Skip to main content

“Aggy Uliniambia Huwezi Kunipenda Nikikataa Kupima Ngoma”-Rammy Galis




Muigizaji Rammy Galis ni moja kati ya mastaa wa Bongo walionyesha kuguswa na kifo cha Agnes Masogange ambaye ni mpenzi wake wa zamani, Rammy Galis ametumia ukurasa wake wa instagram kuandika ujumbe ambao umemuumiza kutokana na taarifa hizi.


“Mkono umekuwa mzitoo hata kuandika maumivu niliyonayoo naona nashindwa . Dunia tambara mbovu , unadeki salama mchana usiku unakua mmbovu umenifunza mengi niliyokua siyajui , ulisema nishkuru mungu watu wakikupenda kwani adui haumjui”


“Miezi 11 tumeishi nashkuru ulinipeleka kupima ( Palestina ) , Nilitokwa na jasho ukanicheka ukaniambia huwez nipenda kama nikikataa kupima magazeti ya udaku walipotaka sababu sikuweza kuweka tofauti zetu hadharani kwani bado moyoni niliamini ipo siku Tungeweza Kumuepusha shetani . Tulikesha Usiku Na Mchana ili Ucheze Filamu Yetu Kwa hisia ” Ukasema Hii Iwe Kumbukumbu Yako Kama Niliwahii Hata Kwenye Kazi Zako Kukusaidia”

“Sasa kwanini filamu yetu tulitunga jina liitwe #HUKUMU ? Ilikuwaje Story ya filamu mwisho unafariki ? kwani tulikua tunatungia iwe kweli Hukumu yako ???? Mungu ndio hakimu wa viumbe vyote katika dunia , umeondoka ghafla sanaa , Na hii pia ni funzo umeniachia #PumzikaSalama #MileleNakuombea#RIPLOVE😢”


Marehemu Agness Masogange enzi za uhai wake aliwahi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na muigizaji Rammy Galis kwa kipindi kifupi kinachotajwa kufikia miezi 11 lakini baadae walachana na kutotaja sababu ya kuachana kwao.




Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "