Skip to main content

CHADEMA YADAI NI ZAIDI YA TRILIONI 1.5 ZILIZOPIGWA



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimefanya mkutano na waandishi wa habari na kuudai kwamba ukiachilia mbali kiwango za zaidi ya shilingi trilioni 1.5 ambazo zilidaiwa na Zitto Kabwe kwamba hazifahamiki zimekwenda wapi katika ripoti ya CAG, kuna kiwango kingine kikubwa cha fedha pia kimetumika hovyo. 

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Uenezi wa Chadema, John Mrema, leo Aprili 18, 2018 katika makao makuu ya Chama hicho, Kinondoni Dar, na kudai kuwa fedha nyingine zilizopotea ni za kwenye mashirika ya umma yakiwemo ya mifuko ya hifadhi za jamii, ununuzi wa ndege na Shirika la Ndege kwa ujumla. Amedai chama chao kitatoa ufafanuzi wa kifungu kwa kifungu kuhusu ripoti hiyo ya CAG. 

“Baada ya sakata hili la trilioni 1.5, kuna wanasiasa hasa wa ccm wanataka kubadilisha mjadala huu na kuanza kusema eti Chadema kuna ufisadi,” alisema John Mrema. 

Hata hivyo, Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji amesema hakuna fedha taslimu kiasi cha shilingi trilioni 1.51 iliyopotea au kutumika kwa matumizi ambayo hayakuidhinishwa na Bunge. 

Pia, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa katika ripoti ambayo alipokea kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad haikuonyesha upotevu wa fedha hizo na kueleza endapo kungebainika kitu kama hicho, basi aliyehusika angechukua hatua kali siku hiyo hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "