Skip to main content

John Heche Azungumza Mazito Baada ya Mdogo Wake Kuuwawa Kikatili na Polisi





Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amefunguka kuwa mpaka sasa haelewi ni kwa vipi mtu anaweza kuuwawa na polisi kwa kuchomwa kisu tena akiwa amefungwa pingu huku akikumbushia tukio la mdogo wake mwingine kujeruhiwa vibaya na polisi ambapo alisababishiwa ulemavu mwaka jana. 

Mbunge Heche amesema kwamba mtu kuchomwa kisu mgongoni ni kudhamiria kuua kwasababu mtu huyo hakuwa anapambana. 

"Nilijua mikononi mwa polisi ni sehemu salama, wiki mbili zilizopita kijana Allen alikufa katika mazingira tata kule Mbeya, Mwanza mama aliyekamatwa na kunyimwa dhamana mtoto wake mchanga alikufa. Leo ni kwangu mdogo wangu ameuwawa kikatili sana mikononi mwa polisi. Maisha yangu yote nimeyatoa kupigania haki ili watu wasionewe, mtuhumiwa asifanywe mkosaji na kuhukumiwa kabla ya vyombo vya sheria kumhukumu,"  Heche. 

Ameongeza " Mwaka jana mdogo wangu mwingine aliumizwa vibaya sana na polisi. IGP Mangu na RPC waliokuwa Tarime walilipa uzito suala hilo lakini walipoondolewa, suala liligeuzwa kisiasa na wale vijana waliokua wamemjeruhi mdogo wangu ambaye mpaka sasa sikio moja halisikii,wakarudishwa kazini kinyemera na kuhamishwa Tarime kama kunikomoa. Mimi nimewahi kutishiwa kuuwawa kituo cha polisi, najisikia maumivu makubwa mno lazima Watanzania wakatae hali hii". 

Pamoja na hayo Mbunge huyo amehoji juu ya ukimya wa Waziri na kuongeza kwamba ni watu wangapi wanakufa na kuumizwa mikononi mwa polisi bila matukio kujulikana wala kutangazwa na kuweka wazi kwamba atazungumza muda ukifika. 


Comments

Popular posts from this blog

Niyonzima Apata Ajali Ya Gari

Haruna Niyonzima KIUNGO wa Simba, Haruna Niyonzima amenusurika katika ajali aliyoipata eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam. Niyonzima amepata ajali hiyo juzi baada ya gari lake kupiga bonde na kupoteza mwelekeo wakati akirejea nyumbani kwake. Taarifa zinaeleza Niyonzima raia wa Rwanda alikuwa mwenyewe kwenye gari na akiwa njiani wakati anarejea nyumbani, akakutana na majanga hayo. Jana Championi  juhudi za kumpata Niyonzima aliyetua nchini kuichezea Yanga akitokea APR ya Rwanda na baada ya kumpata alithibitisha kupata ajali na kusema anamshukuru Mungu kwa kuwa haikuwa ajali kubwa. “Gari lilipoteza mwelekeo wakati nikiwa njiani narejea nyumbani na kuingia kwenye msingi. Bahati nzuri sikuwa katika mwendo mkubwa na kuna mtu alikatiza ghafla, nilipojaribu kumkwepa nikapoteza mwelekeo wakati najitahidi kurudi barabarani, nikapiga bonde gari likanishinda nikaingia msingini. “Haukuwa msingi mrefu, baadaye walikuja watu tukalitoa nikaondoka. Nashukuru sikuumia wala yule mtu sikumgonga

Rais Magufuli aitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ameipandisha hadhi Manispaa ya Mji wa Dodoma na kuwa Jiji, huku akimtaja Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma wa sasa kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo jipya. Dkt. Magufuli amesema hayo leo Alhamisi, Aprili 26, 2018 wakati akihutubia wananchi waliojitokeza katika Viwanja vya Jamhuri, Dodoma wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania. “Lengo la Serikali yetu kuhamia Dodoma lipo pale pale, hatuwezi kurudi nyuma. Sasa hivi zaidi ya watumishi 3,800 wameshahamia, mimi nitahamia Dodoma mwaka huu. Dodoma ndio Makao Makuu. Kwa mamlaka mliyonipa, natangaza rasmi kuanzia leo Aprili 26, 2018, Manispaa ya Dodoma itakuwa Jiji la Dodoma, mkurugenzi wake ataanza kuitwa Mkurugenzi wa Jiji”, amesema Dkt. Magufuli. Aidha, Rais Magufuli amesema maandalizi yote ya kisheria yaanze kutumika katika jiji hilo jipya nalitakuwa Jiji la kipekee kwa sababu lipo katikati ya Tanzania”.

Mama Kanumba Amjibu Wema Baada ya Kukataa Kuigiza Nae.

BAADA ya hivi karibuni staa wa filamu, Wema Sepetu kueleza maneno aliyoelezwa na aliyekuwa msanii wa filamu, marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake kwamba hataki kabisa mama yake mzazi, Flora Mtegoa aigize, mzazi huyo ameibuka na kufungukia ishu hiyo. Akipiga stori na Za Motomoto News, mama Kanumba alisema mwanaye huyo alisema hayo kwa sababu alikuwa akimtunza na kumlipa mshahara kama mfanyakazi lakini kwa sasa hayupo hivyo ndiyo maana ameingia kwenye sanaa ya uigizaji kwa kuwa bila hivyo angegeuka ombaomba jambo ambalo halipendezi. “Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha,” alisema mama Kanumba