Skip to main content

Kijana Akutwa Amejinyonga Jirani Ya Msikiti

Pemba. Katika hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa Ole Mchanga, Mkoa wa Kaskazini Pemba, Azani Abdallah Suleiman (28) amekutwa amejinyonga katika mti uliopo nje ya msikiti wa Machomane, wilayani Chackechake.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Sheikhan Mohamed Sheikhan alisema tukio hilo lilibainika wakati waumini walipofika msikitini saa 11:00 alfajiri kwa ajili ya swala ya Subhi.

Sheikhan alisema baada ya waumini hao kuingia msikitini waliona maiti ya kijana huyo ikining’inia juu ya mti ulio nje ya msikiti huo.

Alisema taarifa za awali zinaeleza kuwa kijana huyo alifika kwa babu yake mkazi wa Machomane, Chakechake na kufanya mazungumza kuhusu mipango yake ya kuoa.

“Tumeambiwa kwamba hakukuwa na maelewano mazuri na babu yake baada ya kumpa taarifa hiyo, ilipofika usiku alimtaka mjukuu wake huyo akapumzike lakini baadaye kijana huyo alikwenda kujinyonga,’’ aliongezea Sheikhan.

Aliitaka jamii hususan wazazi wawe na utaratibu wa kuzungumza lugha nzuri na watoto wao ili kuepusha matukio ya aina hiyo, kwa kuwa yanaweza kupata suluhu ili kuepusha madhara kama hayo.


Kamanda Sheikhan alisema baada ya kuitwa na waumini, polisi walichukua mwili wa marehemu na kuupeleka Hospitali ya Chakechake na kufanyiwa uchunguzi na kwamba, haukuwa na jeraha lolote linaloashiria kupigwa au kuteswa.


Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "