Skip to main content

Mabishano Makali ya Kisheria Yatikisa Kesi ya Nondo Kesi Yaahirisha Hadi Jumatatu


Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imeipiga kalenda kesi ya mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi Jumatatu kutokana na mabishano makali ya kisheria yaliyotokea kortini hapo kati ya pande mbili za utetezi na Jamhuri. 

Akiahirisha kesi hiyo, Hakimu Mkazi John Mpitanjia alisema anajipa muda kwa lengo la kupitia sheria kuhusiana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na shahidi wa pili; kwamba kielelezo chake kipokelewe na mahakama ama la. 

Upande wa uetetezi ukiongozwa na wakili Jebra Kambole akisaidiwa na Chance Luwoga, uliomba mahakama kutopokea hati ya upekuzi kwa madai ina mkanganyiko wa majina na kwamba ni watu wawili tofauti. 

Aidha, utetezi ulipinga hati ya uchunguzi kuwa imekosewa jina la mshitakiwa kwani badala ya kuandika Abdul Mahamud Omary Nondo imesajiliwa kwa jina la Mahmud Omary Nondo. 

Upande huo uliomba kutupiliwa mbali kwa nyaraka hiyo ambayo upande wa Jamhuri ukiongozwa na wakili wa serikali, Alex Mwita akisaidiwa na Pianzia Nchemba umesema cha muhimu ni ujumbe uliopo ndani. 

Mwita alisema huenda nondo alitoa majina mawili tofauli kwa sababu alihojiwa na watu wawili tofauti. 

Hoja ya tatu iliyotolewa na upande wa utetezi ni kwamba ilikuwaje Koplo John kutumia kifungu cha 10 (3) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA)Sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 kuthibitisha waraka huo ili hali kabla alisajili kwa kutumia kifungu cha 34 (b) cha Sheria ya Ushahidi. 

Awali, shahidi wa kwanza ambaye ni E.3232 Koplo Salim aliiambia mahakama kwamba Nondo aliwasili kituo cha polisi majira ya moja usiku na kuchukuliwa maelezo ya awali. 

Alidai Nondo alisema amefika kituoni kutoa malalamiko ya kutekwa na watu wasiojulika na kutelekezwa katika Kiwanda cha Pareto Pct Mafinga. 

Kolpo Salim aliiambia mahakama kuwa Nondo aliiambia Polisi kwamba alitekwa jijini Dar es Salaam na kusafirishwa hadi Mafinga Iringa na ndipo alimkabidhi kwa mpelelezi Koplo John mwenye namba E.7665 ambaye ni shahidi wa pili katika kesi hiyo, ili aweze kumchukua maelezo kwa kina kuhusiana na malalamiko yake. 

Hata hivyo, mahakama ilipokea vielelezo ambavyo Nondo alivikabidhi Kituo cha Polisi Mafinga ambavyo ni kompyuta mpakato aina ya Dell, kadi ya mawasiliano (bussness card), kadi ya benki, simu ya kiganjani aina ya Itel na kitambulisho cha chuo. 

Awali, Hakimu Mpitanjia alisema kabla ya mashahidi kutoa ushahidi wao inabidi mtuhumiwa kusomewa mashataka yake yanayomkabili na Nondo alikana mashtaka hayo. 

Jamhuri imekusudia kuleta mashahidi watano zaidi ambapo jana ni mashahidi wawili tu waliopanda kizimbani kutokana na kutofikia muafaka baada ya pande mbili hizo kunyukana kwa kutumia vifungu vya sheria. 

Jamhuri imekusudia kuwaleta pia kutoa ushahidi Koplo Salum, Veronica Fredy ambaye ni mpenzi wake Nondo, Alphonce Mwamule, Koplo Abdulkadir na mtu kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Tigo. 

Nondo ameshitakiwa kwa makosa mawili ya kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya kompyuta na kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma ambaye ni askari polisi Koplo Salim wa Kituo cha Polisi Mafinga wilayani Mufindi. 

Ilidaiwa kwamba Machi 7, mwaka huu akiwa Ubungo jijini Dar es Salaam, mshitakiwa alitenda kosa la kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya kompyuta akitumia simu ya kiganjani yenye No. 0659366125 kinyume cha Sheria ya Makosa ya Mtandao na kusambaza katika mitandao ya kijamii.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "