Skip to main content

Mabishano Makali ya Kisheria Yatikisa Kesi ya Nondo Kesi Yaahirisha Hadi Jumatatu


Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imeipiga kalenda kesi ya mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo hadi Jumatatu kutokana na mabishano makali ya kisheria yaliyotokea kortini hapo kati ya pande mbili za utetezi na Jamhuri. 

Akiahirisha kesi hiyo, Hakimu Mkazi John Mpitanjia alisema anajipa muda kwa lengo la kupitia sheria kuhusiana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na shahidi wa pili; kwamba kielelezo chake kipokelewe na mahakama ama la. 

Upande wa uetetezi ukiongozwa na wakili Jebra Kambole akisaidiwa na Chance Luwoga, uliomba mahakama kutopokea hati ya upekuzi kwa madai ina mkanganyiko wa majina na kwamba ni watu wawili tofauti. 

Aidha, utetezi ulipinga hati ya uchunguzi kuwa imekosewa jina la mshitakiwa kwani badala ya kuandika Abdul Mahamud Omary Nondo imesajiliwa kwa jina la Mahmud Omary Nondo. 

Upande huo uliomba kutupiliwa mbali kwa nyaraka hiyo ambayo upande wa Jamhuri ukiongozwa na wakili wa serikali, Alex Mwita akisaidiwa na Pianzia Nchemba umesema cha muhimu ni ujumbe uliopo ndani. 

Mwita alisema huenda nondo alitoa majina mawili tofauli kwa sababu alihojiwa na watu wawili tofauti. 

Hoja ya tatu iliyotolewa na upande wa utetezi ni kwamba ilikuwaje Koplo John kutumia kifungu cha 10 (3) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA)Sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 kuthibitisha waraka huo ili hali kabla alisajili kwa kutumia kifungu cha 34 (b) cha Sheria ya Ushahidi. 

Awali, shahidi wa kwanza ambaye ni E.3232 Koplo Salim aliiambia mahakama kwamba Nondo aliwasili kituo cha polisi majira ya moja usiku na kuchukuliwa maelezo ya awali. 

Alidai Nondo alisema amefika kituoni kutoa malalamiko ya kutekwa na watu wasiojulika na kutelekezwa katika Kiwanda cha Pareto Pct Mafinga. 

Kolpo Salim aliiambia mahakama kuwa Nondo aliiambia Polisi kwamba alitekwa jijini Dar es Salaam na kusafirishwa hadi Mafinga Iringa na ndipo alimkabidhi kwa mpelelezi Koplo John mwenye namba E.7665 ambaye ni shahidi wa pili katika kesi hiyo, ili aweze kumchukua maelezo kwa kina kuhusiana na malalamiko yake. 

Hata hivyo, mahakama ilipokea vielelezo ambavyo Nondo alivikabidhi Kituo cha Polisi Mafinga ambavyo ni kompyuta mpakato aina ya Dell, kadi ya mawasiliano (bussness card), kadi ya benki, simu ya kiganjani aina ya Itel na kitambulisho cha chuo. 

Awali, Hakimu Mpitanjia alisema kabla ya mashahidi kutoa ushahidi wao inabidi mtuhumiwa kusomewa mashataka yake yanayomkabili na Nondo alikana mashtaka hayo. 

Jamhuri imekusudia kuleta mashahidi watano zaidi ambapo jana ni mashahidi wawili tu waliopanda kizimbani kutokana na kutofikia muafaka baada ya pande mbili hizo kunyukana kwa kutumia vifungu vya sheria. 

Jamhuri imekusudia kuwaleta pia kutoa ushahidi Koplo Salum, Veronica Fredy ambaye ni mpenzi wake Nondo, Alphonce Mwamule, Koplo Abdulkadir na mtu kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Tigo. 

Nondo ameshitakiwa kwa makosa mawili ya kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya kompyuta na kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma ambaye ni askari polisi Koplo Salim wa Kituo cha Polisi Mafinga wilayani Mufindi. 

Ilidaiwa kwamba Machi 7, mwaka huu akiwa Ubungo jijini Dar es Salaam, mshitakiwa alitenda kosa la kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya kompyuta akitumia simu ya kiganjani yenye No. 0659366125 kinyume cha Sheria ya Makosa ya Mtandao na kusambaza katika mitandao ya kijamii.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt...

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny...