Skip to main content

Mfaransa Simba Awapigia Magoti Waamuzi

Kocha Mkuu wa Simba, Mfaransa, Pierre Lechantre (katikati). KOCHA Mkuu wa Simba, Mfaransa, Pierre Lechantre amefunguka kuwa amekuwa akipata wakati mgumu katika mechi za Ligi Kuu Bara zilizosalia kutokana na washambuliaji wake, tegemeo, John Bocco na Mganda, Emmanuel Okwi kukamiwa na mabeki wa timu pinzani.

Katika ligi hiyo, Simba kwa sasa inaongoza ikiwa na pointi 52, ambazo ni sita zaidi ya Yanga inay­oshika nafasi ya pili nyuma ya Azam inayoshika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 45.

Simba imefikisha pointi hizo baada ya juzi Jumatatu kufanikiwa kuifunga Mti­bwa Sugar bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Akizungumza na Cham­pioni Jumatano, Lechantre amesema kuwa amekuwa akipata wakati mgumu kutokana na wachezaji hao kupata majeraha ya mara kwa mara kutokana na ku­kamiwa na mabeki wa timu pinzani jambo ambalo linaweza kuvuruga mipango yake ya ubingwa.

Kocha huyo amekwenda mbali zaidi kwa ku­waomba waamuzi kuongeza umakini wao kwa wachezaji wake hao ili waweze kufikia malengo ya msimu huu kwa kuwa safu ya ushambuliaji ndiyo tegemezi katika ufun­gaji wa mabao.

“Kiwango cha Bocco tangu atoke kwenye majeruhi kimezidi kupanda, amekuwa moto maana ukiangalia amesaidia kufunga ma­bao ya kutosha kwenye mechi za hivi karibuni.

“Lakini bado nimekuwa na hofu ya kuweza ku­maliza nao msimu wakiwa wazima kwa sababu, yeye na Okwi wamekuwa wakichezewa rafu kwa kuwa wana­kamiwa na mabeki wa timu pinzani kitu ambacho mara nyingi kinavuruga mipango yetu.

“Nadhani kuna haja ya waamuzi kuongeza umakini kwa sababu, soka siyo mchezo wa uadui lakini mabeki wa timu nyingi hufanya kusudi kabisa na ukiangalia ni wachezaji muhimu kwenye kikosi cha kwanza maana tunataka kushinda mechi zote,” alisema Lechantre.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt...

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny...