Skip to main content

Mmoja afariki na wawili kujeruhiwa vibaya kisa ugomvi wa mapenzi



MTU mmoja amefariki na wawili kujeruhiwa vibaya kwa kukatana mapanga mkoani Mara, kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Juma Ndani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika kijiji cha Kingongo wilayani Serengeti.Kamanda Ndani alimtaja marehemu kuwa ni Kibure Samwel (39) ambaye alichomwa kisu tumboni na kifuani.

Aidha aliwataja majeruhi kuwa ni Nyanga'anyi Waitara (44), ambaye alijeruhiwa mkononi na Munge Samwel (44) aliyejeruhiwa kwenye paja.

Akisimulia tukio hilo, Kamanda Ndani alisema chanzo cha ugomvi huo ni wivu wa mapenzi ambapo mwamamke (jina limehifadhiwa) alikuwa mke wa Waitara na sasa ameolewa na Munge.

Alisema tangu mwanamke huyo aolewe na Munge kumekuwa na mgogoro baina yao na siku ya tukio walianza kutoleana maneno makali na baadaye kuanza kupigana kwa kutumia mapanga.

Kamanda Ndani alieleza kuwa katika ugomvi huo aliyefariki ni mdogo wa Munge ambaye alipofika kwenye tukio alimkuta kaka yake anashambuliwa na Waitara.

Kamanda Ndani alisema baada ya kuona hivyo, akaamua kuchukua panga ili kumsaidia kaka yake lakini Waitara alimuwahi na kumchoma kisu tumboni na kifuani na kufariki.

"Aliyefariki ni mdogo wake Munge Samwel ambaye katika ugomvi huo alifika kwenye tukio na kukuta kaka yake anashambuliana kwa silaha na Waitara, akaamua kuchukua panga kumsaidia ndipo mtuhumiwa akamchoma tumboni kisha kifuani na kufariki," alisema Kamanda Ndani.

Naye Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kirenero, Joseph Mwita alisema mgogoro huo ni wa muda mrefu ambapo Waitara alimshutumu Munge kuwa ndiye chanzo cha mgogoro wa ndoa yake na kusababisha mke wake kudai talaka.

Alisema Waitara alikataa kurudishiwa mahari na Munge ili amchukue mke wake kwa madai kuwa ameshazaa naye watoto watatu.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "