Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, amesema ili kujenga taifa lenye nguvu ni lazima kuwepo na hoja zinazokinzana huku akiwataka watendaji wa Serikali kufanya kazi za kuwatumikia wananchi. Mch. Msigwa ameyasema hayo Bungeni jana wakati akizungumzia masuala ya Utawala Bora nchini na kudai kuwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo, ni kama amesahau kazi yake na badala yake kutumia muda mwingi kuwajibu maaskofu. “Badala ya kumtua mama ndoo, Prof. Kitila Mkumbo amekazana kuwajibu maaskofu ambao wanashughulika na roho za watu,” alisema Msigwa.
Mkoa wa Kigoma uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...
Comments
Post a Comment