Skip to main content

Ofisa Chuo Kikuu asimamishwa Kazi kwa kumdhalilisha kijinsia Mwanafunzi

KISUZE EDWARD ambaye ni Ofisa Utawala Mwandamizi Ofisi ya Usajili wa Wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda, amesimamishwa kazi kwa kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike. Barua ya kusimamishwa kazi.

 Barua iliyotolewa na Kaimu Mkuu wa chuo hicho, Prof. William Bazeyo, kwenda kwa mtuhumiwa, imemsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi wa tukio hilo ambapo pia hatakiwi kufika katika ofisi hizo.

Mlalamikaji, Njoroge Racheal, aliiambia polisi kwamba Kisuze alimbusu kwa nguvu kwenye mapaja yake na kumshika sehemu za siri.

 Mwanafunzi huyo alitumia simu yake kupiga picha kadhaa za tukio hilo ambazo amezifikisha polisi.

Katika maelezo aliyoyatoa polisi, mwanafunzi huyo alisema tukio hilo lilitokea katika chumba cha ofisi ya Kisuze alipokwenda kuchukua matokeo yake ya awali na barua ya uthibitisho chuoni.

Wakati anavitazama hati hizo, mtuhumiwa alimkamata na kumlaza kwenye makabati ya mafaili, akamnyonya maziwa na mapaja, na kumwingiza vidole sehemu zake za siri.

Ni wakati hayo yanatokea, alitumia simu yake kupiga picha za tukio hilo na kumtishia kumshitaki ndipo mtuhumiwa alipomwachia akaondoka hapo akilia.




Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "