Skip to main content

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT).

Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo.

Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika.

Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka.

“Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,”alisema Mwita.

Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mto Msimbazi uweze kuwa na nafasi kubwa ya kusafirisha maji hadi baharini.

Meya alisema jambo hilo linaweza kupunguza mafuriko katika eneo la Jangwani na maeneo karibu na mto huo.

Alisema fedha za upanuzi huo zimekwisha kutolewa, kilichobaki ni utekelezaji wa mradi kuanzia daraja la Salendar hadi Pugu.

“Awamu ya kwanza ya mradi itaanzia Salendar hadi Kigogo, jambo ambalo linaweza kupunguza ukubwa wa tatizo la mafuriko kwa wakazi wa Jangwani na maeneo jirani ya mto Msimbazi,” alisema.

Vilevile, Meya Mwita alisema Serikali Kuu imetoa shilingi bilioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa çha mabasi yaendayo mikoani, kitakachojengwa Mbezi Mwisho.

Alisema licha ya kutolewa kiasi hicho cha fedha, jiji limetoa shilingi bilioni nane kwa ajili ya kuwalipa fidia wananchi ambao maeneo yao yatachukuliwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

“Tunatarajia kupata ekari 24 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha Mbezi Mwisho, ujenzi ambao utaanza wakati wowote kuanzia sasa. Mkakati uliopo ni kuwalipa fidia wananchi wa eneo lile tuweze kuendeleza mradi,” alisema.

Alisema mradi huo utachukua miaka miwili kukamilika na ndani yake kutakua na maduka na nyumba za kulala wageni, jambo ambalo linaweza kuwasaidia kuongeza mapato.

Alisema mwaka huu katika makusanyo yake ya kila mwaka, halmashauri imeingiza shilingi bilioni 22 ambazo zitatumika kwa mambo mbalimbali yakiwamo uendelezaji wa miradi.

Chanzo: Swahili Times
========

Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kupeleka kwenye kituo cha mabasi ya mikoani Ubungo UBT, kutokana na eneo hilo la Jangwani kujaa maji kila mara wakati mvua zinaponyesha.


Comments

Popular posts from this blog

Niyonzima Apata Ajali Ya Gari

Haruna Niyonzima KIUNGO wa Simba, Haruna Niyonzima amenusurika katika ajali aliyoipata eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam. Niyonzima amepata ajali hiyo juzi baada ya gari lake kupiga bonde na kupoteza mwelekeo wakati akirejea nyumbani kwake. Taarifa zinaeleza Niyonzima raia wa Rwanda alikuwa mwenyewe kwenye gari na akiwa njiani wakati anarejea nyumbani, akakutana na majanga hayo. Jana Championi  juhudi za kumpata Niyonzima aliyetua nchini kuichezea Yanga akitokea APR ya Rwanda na baada ya kumpata alithibitisha kupata ajali na kusema anamshukuru Mungu kwa kuwa haikuwa ajali kubwa. “Gari lilipoteza mwelekeo wakati nikiwa njiani narejea nyumbani na kuingia kwenye msingi. Bahati nzuri sikuwa katika mwendo mkubwa na kuna mtu alikatiza ghafla, nilipojaribu kumkwepa nikapoteza mwelekeo wakati najitahidi kurudi barabarani, nikapiga bonde gari likanishinda nikaingia msingini. “Haukuwa msingi mrefu, baadaye walikuja watu tukalitoa nikaondoka. Nashukuru sikuumia wala yule mtu sikumgonga

Rais Magufuli aitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ameipandisha hadhi Manispaa ya Mji wa Dodoma na kuwa Jiji, huku akimtaja Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma wa sasa kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo jipya. Dkt. Magufuli amesema hayo leo Alhamisi, Aprili 26, 2018 wakati akihutubia wananchi waliojitokeza katika Viwanja vya Jamhuri, Dodoma wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania. “Lengo la Serikali yetu kuhamia Dodoma lipo pale pale, hatuwezi kurudi nyuma. Sasa hivi zaidi ya watumishi 3,800 wameshahamia, mimi nitahamia Dodoma mwaka huu. Dodoma ndio Makao Makuu. Kwa mamlaka mliyonipa, natangaza rasmi kuanzia leo Aprili 26, 2018, Manispaa ya Dodoma itakuwa Jiji la Dodoma, mkurugenzi wake ataanza kuitwa Mkurugenzi wa Jiji”, amesema Dkt. Magufuli. Aidha, Rais Magufuli amesema maandalizi yote ya kisheria yaanze kutumika katika jiji hilo jipya nalitakuwa Jiji la kipekee kwa sababu lipo katikati ya Tanzania”.

Mama Kanumba Amjibu Wema Baada ya Kukataa Kuigiza Nae.

BAADA ya hivi karibuni staa wa filamu, Wema Sepetu kueleza maneno aliyoelezwa na aliyekuwa msanii wa filamu, marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake kwamba hataki kabisa mama yake mzazi, Flora Mtegoa aigize, mzazi huyo ameibuka na kufungukia ishu hiyo. Akipiga stori na Za Motomoto News, mama Kanumba alisema mwanaye huyo alisema hayo kwa sababu alikuwa akimtunza na kumlipa mshahara kama mfanyakazi lakini kwa sasa hayupo hivyo ndiyo maana ameingia kwenye sanaa ya uigizaji kwa kuwa bila hivyo angegeuka ombaomba jambo ambalo halipendezi. “Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha,” alisema mama Kanumba