Skip to main content

Posts

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Recent posts

Rais Trump kukutana na rais Moon Mei 22

Rais Donald Trump anatarajia kukutana na rais wa Korea Kusini Moon Jae In ifikapo 22 Mei.  Viongozi hao wawili watakutana katika ikulu ya White House nchini Marekani.  Msemaji wa White House Sarah Sanders ametoa maelezo kuhusu mkutano huo na kusema kuwa Korea Kusini ina uhusiano mzuri na Marekani.  Trump ambae natarajia kukutana na Moon kwa mara ya tatu sasa,anaamini mkutano huo utasaidia katika kudumisha mahusiano kati ya mataifa hayo amwili.  Trump vilevile anatarajia kukutana na Kim Jong Un hivi karibuni.

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny

Polisi abakwa alipokwenda kumkamata mbakaji

Askari Polisi mmoja wa kike huko  Yorkshire Kusini, nchini England  ameripoti kubakwa na mwanaume ambaye alikwenda kumkamata akiwa na askari mwingine kwa makosa ya jaribio la kubaka. Mwanaume huyo alikuwa akihisiwa kufanya vitendo hivyo vya  kujaribu kubaka watoto wa kike  na ndipo askari huyo alipokwenda na mwenzie kumkamata ili afikishwe polisi. Inaelezwa kuwa mwanamume huyo tayari amekwisha kamatwa na amefungulia mashtaka ya  kujaribu kubaka, shambulio, unyanyasaji wa kijinsia na uharibifu wa makosa ya jinai .

Rais Magufuli aomba msaada Serikali ya Denmark

Rais John Magufuli ameiomba Serikali ya Denmark kusaidia ujenzi wa kipande cha barabara ya kilomita 11 katika Mkoa wa Iringa ili kuwezesha malori kutopita katikati ya mji huo ikiwa ni pamoja na kupunguza ajali zinazotokea.  Rais Magufuli ombi hilo wakati akizindua barabara ya Iyovi – Iringa – Mafinga yenye urefu wa kilomita 218 iliyojengwa kwa mkopo nafuu kutoka serikali ya Denmark na kugharimu Sh283 bilioni.  Akitoa maelezo wakati akiomba msaada huo Dk. Magufuli amesema mpango huo ulikuwepo tangu alipokuwa wizara ya ujenzi na kufafanua kwamba malori yanayopita katikati ya mji wa Iringa yamekuwa yakisababisha ajali ndani ya mji wa huo.  “Nakuomba Balozi, hili mlichukue kama la urgent, mkitusaidia kama mkopo sisi tuko tayari, mkitupa kama msaada tutashukuru zaidi. Kwa hiyo tunaomba utufikishie hili, ikiwezekana barabara hiyo tutaiita Pamela Road,” amesema  Mbali na hayo Rais ameweka wazi kwamba "Ujenzi wa barabara hii umegharimu bilioni 283.71 nimekopa kutoka Denmark, mb

Mwita Waitara: Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure

Mbunge wa Ukonga (CHADEMA) Mh. Mwita Waitara amehoji uamuzi wa serikali kutangaza kutoa elimu bure licha ya changamoto ambazo bado zinaikumba sekta hiyo nchini na kutaka wananchi waingie gharama za kuchangia elimu isipokua kwa familia maskini.  Waitara amesema hayo jana bungeni Mei 02, 2018 wakati wa kuchangia bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kuongeza kwamba Tanzania hakuna elimu ya bure bali serikali imepunguza gharama kwa kufuta ada tu.  “Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure, kuna elimu iliyopunguzwa gharama zake, serikali ilichofanya imeondoa ada lakini mambo mengine yatabaki, natukubaliane mheshimiwa Mwenyekiti haiwezekani taifa hili kila kitu kikatolewa bure watoto watakua wazembe na walemavu” alisema Waitara  Waitara ameongeza kuwa kitendo cha serikali kutangaza elimu bure kinadumaza wananchi na kushindwa kutimiza majukumu yao kama wazazi katika jukumu la kusimamia watoto kielimu na itapelekea Tanzania kuwa ni taifa la wat

Ajisalimisha Polisi baada ya Mzigo alioiba kunasa mabegani

KIJANA Frank Japhet (23), mkazi wa Mbezi, Dar es Salaam, amelazimika kujisalimisha katika Kituo cha Polisi Mlandizi, Kibaha, Pwani, baada ya mzigo wa mahindi unaokadiriwa kuwa na uzito wa kilogramu 20, anaodaiwa kuuiba kung’ang’ania mabegani.  Wakati akihojiwa kituoni hapo, mtuhumuwa huyo amesema mzigo huo, uliofungwa kwenye kiroba aliuiba kwa mama mmoja eneo la Mtaa wa Nyambwiro, Mlandizi, Kibaha, mkoani Pwani majira ya saa 7.00 usiku wa kuamkia leo Mei 3, 2018, akaongeza kwamba aliondoka na mzigo huo hadi eneo la Stendi ya Mlandizi alipokuwa auache kwa mwenzake ili arudie mzigo mwingine, ambapo mzigo huo uling’ang’ania kichwani.  Ameendelea kusema kwamba alijitahidi kufanya kila aliloweza ili mzigo huo utoke kichwani ikiwa ni pamoja na kulala ili akinyanyuka ubaki chini lakini aliponyanyuka, alinyanyuka nao kichwani! Baada ya kuzunguka nao kwa muda mrefu, alidai alichoka hivyo akalazimika kujisalimisha polisi ili asije akauawa na raia wenye hasira watakapobaini kuwa ni mwizi