Skip to main content

Mwita Waitara: Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure




Mbunge wa Ukonga (CHADEMA) Mh. Mwita Waitara amehoji uamuzi wa serikali kutangaza kutoa elimu bure licha ya changamoto ambazo bado zinaikumba sekta hiyo nchini na kutaka wananchi waingie gharama za kuchangia elimu isipokua kwa familia maskini. 

Waitara amesema hayo jana bungeni Mei 02, 2018 wakati wa kuchangia bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kuongeza kwamba Tanzania hakuna elimu ya bure bali serikali imepunguza gharama kwa kufuta ada tu. 

“Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure, kuna elimu iliyopunguzwa gharama zake, serikali ilichofanya imeondoa ada lakini mambo mengine yatabaki, natukubaliane mheshimiwa Mwenyekiti haiwezekani taifa hili kila kitu kikatolewa bure watoto watakua wazembe na walemavu” alisema Waitara 

Waitara ameongeza kuwa kitendo cha serikali kutangaza elimu bure kinadumaza wananchi na kushindwa kutimiza majukumu yao kama wazazi katika jukumu la kusimamia watoto kielimu na itapelekea Tanzania kuwa ni taifa la watu wavivu. 

Serikali ya awamu ya tano ilianza kutoa elimu ya bure katika ngazi ya awali, msingi na sekondari kuanzia mwaka 2016 ikiwa ni utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo ya 2014 na ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 2015. 

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "