Skip to main content

Serikali Yataifisha Basi na Magari ya Kifahari

Serikali imetaifisha dhahabu ya mabilioni ya shilingi na magari ya kifahari kutokana na wahusika wake kukamatwa na kuhukumiwa kwa makosa ya rushwa katika mwaka huu wa fedha.

Pia imetaifisha, pikipiki, mafuta, mashine za kuhesabia fedha na basi la abiria lililokuwa linatumika kusafirisha meno ya tembo.

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Paramagamba Kabudi, aliyasema hayo jana alipowasilisha bungeni mjini hapa hotuba ya makadirio ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha.

Alibainisha kuwa katika mwaka huu wa fedha, mali zilizotaifishwa kwa ujumla wake zinakadiriwa kuwa na thamani ya Sh. bilioni 5.685. Waziri huyo alisema Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ilipokea majalada 683 ya tuhuma za rushwa kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru).

Prof. Kabudi alisema kati ya hayo, majalada 288 yaliandaliwa hati za mashtaka na 275 yalirudishwa Takukuru kwa uchunguzi zaidi.

Alisema majalada 115 yako katika hatua mbalimbali yakifanyiwa kazi na mengine matano yalifungwa.

"Washtakiwa waliotiwa hatiani walipewa adhabu mbalimbali zikiwamo vifungo, faini na mali kutaifishwa ambapo jumla ya Sh. bilioni 4.484 zilitozwa kama faini kutoka kwa washtakiwa," alisema na kuongeza: "Mali zilizotaifishwa ni pamoja na kilogramu 24.5 za dhahabu zenye thamani ya Sh. bilioni 2.012 na fedha za kigeni kutoka mataifa 15 zenye thamani ya Sh.milioni 908.092. "Mali zingine zilizotaifishwa ni magari matano ya kifahari aina ya Range Rover Vogue na moja aina ya Audi yaliyokamatwa katika Bandari ya Dar es Salaam yakisafirishwa kama nguo za mitumba, pikipiki 34, mafuta, mashine za kuhesabia fedha na basi la abiria lililokuwa linasarifirisha meno ya tembo."

Prof. Kabudi alisema mwaka huu wa fedha pia mali za vyama vya ushirika vya Mwanza (Nyanza Cooperative Union) na Shinyanga (Shirecu) zikiwamo nyumba, viwanja na viwanda, zimerejeshwa serikalini kutoka mikononi mwa watu ambao walizichukua bila kufuata utaribu wa kisheria.

Waziri huyo pia alisema mwaka huu wa fedha kulikuwa na mashauri sita yanayohusu ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi yaliyoshughulikiwa.

Alisema kuwa kati yake, mashauri manne yalikamilika kwa watuhumiwa kutiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu za kifungo cha kati ya miaka minne hadi 20 na mashauri mawili yaliyobaki yanaendelea kusikilizwa.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt...

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny...