Skip to main content

SIDO Kigoma hatarini, Miundombinu si rafiki

Kiwanda cha SIDO mkoani Kigoma kinachojihusisha na uchakataji wa mazao yatokanayo na Mchikichi kipo hatarini kupunguza uzalishaji kutokana na kutokuwa na miundombinu bora.

Meneja wa SIDO mkoani Kigoma Gelevas Mtahaba alielezea alikiri kuwepo kwa changamoto hizo zinazoikabili kiwanda hicho ambacho hutumiwa na wajasiliamali wengi.

“SIDO inategemewa mkoani hapa na wajasiliamali wa zao hili la mchikichi ndio kitega uchumi lakini bado zao hilo halina ubora kuweza kuzalisha mafuta mengi kutokana na wakulima wa zao hili kutokua na elimu juu ya zao hili,” alisema Mtahaba.

Mtahaba alisema ikiwa Sera ya Awamu ya Tano ni Tanzania ya Viwanda mkoa huu uko nyuma katika viwanda japokua wanategemea zao la mchikichi toka enzi za wakoloni, ni vyema wananchi wakaanzisha vikundi vidogovidogo ili waweze kupata mikopo yenye riba nafuu kwa lengo la kuanzisha viwanda vidogo.

Alisema kiwanda hicho cha SIDO ina jumla ya wajasiliamali 300 kutoka kigoma na maeneo ya jirani ambapo hulipa ushuru na kuingiza kipato katika serikali.

Naye moja kati ya wajasiliamali Hamisi Mengi, alisema wanakabilia wa changamoto ya maji machafu yanayotuama katika kiwanda hicho kusababisha harufu mbaya na kuwa kero kwa wajasiliamali katika eneo hilo.

Mengi, alisema usafiri pia ni changamoto inayo wakabili kutoka shambani hadi kiwandani hapo, jambo ambalo linawakatisha tamaa wajasiliamali wengi na wengine kuachana na biashara hiyo.

Alisema ni vyema Serikali ikawekeza katika zao hilo kwani ni zao ambalo huzalisha mafuta ya mawese na sabuni ambazo hutegemewa na ndani ya nchi na kupanua soko katika zao hilo kuliko kuagiza bidhaa nyingine kutoka nchi za nje.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "