Skip to main content

SIDO Kigoma hatarini, Miundombinu si rafiki

Kiwanda cha SIDO mkoani Kigoma kinachojihusisha na uchakataji wa mazao yatokanayo na Mchikichi kipo hatarini kupunguza uzalishaji kutokana na kutokuwa na miundombinu bora.

Meneja wa SIDO mkoani Kigoma Gelevas Mtahaba alielezea alikiri kuwepo kwa changamoto hizo zinazoikabili kiwanda hicho ambacho hutumiwa na wajasiliamali wengi.

“SIDO inategemewa mkoani hapa na wajasiliamali wa zao hili la mchikichi ndio kitega uchumi lakini bado zao hilo halina ubora kuweza kuzalisha mafuta mengi kutokana na wakulima wa zao hili kutokua na elimu juu ya zao hili,” alisema Mtahaba.

Mtahaba alisema ikiwa Sera ya Awamu ya Tano ni Tanzania ya Viwanda mkoa huu uko nyuma katika viwanda japokua wanategemea zao la mchikichi toka enzi za wakoloni, ni vyema wananchi wakaanzisha vikundi vidogovidogo ili waweze kupata mikopo yenye riba nafuu kwa lengo la kuanzisha viwanda vidogo.

Alisema kiwanda hicho cha SIDO ina jumla ya wajasiliamali 300 kutoka kigoma na maeneo ya jirani ambapo hulipa ushuru na kuingiza kipato katika serikali.

Naye moja kati ya wajasiliamali Hamisi Mengi, alisema wanakabilia wa changamoto ya maji machafu yanayotuama katika kiwanda hicho kusababisha harufu mbaya na kuwa kero kwa wajasiliamali katika eneo hilo.

Mengi, alisema usafiri pia ni changamoto inayo wakabili kutoka shambani hadi kiwandani hapo, jambo ambalo linawakatisha tamaa wajasiliamali wengi na wengine kuachana na biashara hiyo.

Alisema ni vyema Serikali ikawekeza katika zao hilo kwani ni zao ambalo huzalisha mafuta ya mawese na sabuni ambazo hutegemewa na ndani ya nchi na kupanua soko katika zao hilo kuliko kuagiza bidhaa nyingine kutoka nchi za nje.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt...

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny...