Skip to main content

Wabunge waililia serikali kuhusu uhaba wa wauguzi na madaktari


Wabunge wameiomba serikali iliangalie kwa jicho la pekee tatizo la uhaba wa watumishi wa afya, hususani wauguzi na madaktari bingwa katika vituo, zahanati na hospitali na kulipatia ufumbuzi.

Pamoja na hayo, wabunge pia wamebainisha juu ya umuhimu wa serikali kuongeza jitihada za kutekeleza mpango wake wa kujenga zahanati katika kila kata kwa kuwa bado yapo maeneo ambayo hayana zahanati na kulazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya. Wabunge waliyasema hayo bungeni Dodoma jana wakati wakichangia mjadala wa kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ya mwaka 2018/19.

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule (Chadema) alisema wilayani Kilosa hali ya upungufu wa watumishi ni kubwa kwani hadi sasa kuna mahitaji ya watumishi 1,025 na waliopo ni 474 tu sawa na asilimia 46. Alisema tatizo hilo limeongezewa uzito zaidi na utaratibu wa kupunguza watumishi wenye vyeti feki na hivyo kusababisha uhaba wa madaktari na wauguzi katika vituo vya afya, zahanati na hospitali ya Kilosa.

Naye Mbunge wa Kuteuliwa, Salma Kikwete (CCM) alisema afya ndio msingi wa maendeleo katika nchi yoyote endapo kuna ukosefu wa afya, uchumi wa eneo husika utapungua kwa kukosa nguvu kazi. Hata hivyo, alisema Mkoa wa Lindi mpaka sasa haujafahamu hatma yake ya kuwa na hospitali ya mkoa na wilaya, kwani hospitali iliyopo ya Sokoine imekuwa ikiitwa ya mkoa na wilaya na hivyo kuleta mkanganyiko.

“Pamoja na mkanganyiko huu bado mkoa huu una tatizo kubwa la uhaba wa wataalamu wa afya. Ni asilimia 28 pekee ya wataalamu wa afya ndio wapo Lindi na hivyo kuwa na upungufu wa asilimia 72 ya wataalamu hao,” alisisitiza Mama Kikwete. Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Makilagi (CCM), alisisitiza juu ya umuhimu wa serikali kuliangalia tatizo la uhaba wa wataalamu wa afya kwa kuwa hospitali nyingi nchini zinakabiliwa na hali mbaya ya uhaba wa watumishi hao.

Kwa upande wake, Mariam Kisangi (Viti Maalumu - CCM), aliiomba serikali kuboresha hali ya matibabu katika Hospitali ya Mloganzila nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kwa kuiongozea wataalamu zaidi wakiwemo madaktari bingwa na wauguzi kwa kuwa kwa sasa hospitali hiyo inazidiwa na wagonjwa.

Mbunge wa Vunjo (NCCRMageuzi), James Mbatia alisema ni wakati sasa wa serikali kuanza kushirikisha sekta binafsi na wawekezaji wakubwa wa ndani na nje ya nchi ili wawekeze katika sekta ya afya na kuongeza ubora wa huduma za afya nchini. “Tuwe wakweli japo wataalamu wetu wanafanya kazi kubwa, hatujawawezesha kibajeti ili waweze kufanya kazi yao. Serikali inabidi iweke mazingira rafiki na motisha kwa sekta binafsi wavutiwe ili wawekeze kwenye sekta hii...”

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt...

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny...