Skip to main content

Waziri Mkuu awataka Viongozi kuacha tabia ya kuingiza siasa kwa watu wanaoishi mabondeni

Serikali ya Tanzania kupitia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Wabunge na viongozi wengine kuacha tabia ya kuingiza siasa kwa watu wanaoishi mabondeni kwa kuwatetea kutohama maeneo hayo jambo ambalo linawapelekea kupata madhara pindi mvua kubwa zinaponyesha kama ilivyo sasa.

Waziri Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Aprili 19, 2018 Bungeni jijini Dodoma kwenye kikao cha 13 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu swali la Mbunge Abdalla Mtolea ambapo alitaka kujua serikali ina mpango gani wa kuhakikisha madhara yanayojitokeza katika jiji la Dar es Salaam na mvua kudhibitiwa? "kupitia Manispaa za jiji la Dar es Salaam na serikali yake kupitia wizara zake zinazo mipango ya kuboresha miundombinu katika miji yetu katika makao makuu ya mikoa na maeneo yote yale yanayokaliwa na watu wengi ikiwepo DSM.


Tunayo miradi sasa ambayo itaweza kuboresha miundombinu ikiwepo na bonde la Msimbazi ambalo linaleta madhara mengi... Mara kadhaa tumeshuhudia mvua hizi zinapoleta madhara kwa wale walioko mabondeni pamoja na serikali kuwaambia waondoke mabondeni tumekuwa tukiingilia sana utendaji kwa kuingiza siasa za kuwataka watu wabaki huku wengine wakijafanya wanawaonea huruma na kushindwa kutoka katika mabonde kutokana na utetezi unaotoka kwa watu wenye mapenzi yao binafsi", amesema Majaliwa. Waziri Mkuu ameendelea kwa kusema..

"Nitoe wito kama ambavyo tunaendelea kutoa wito na Waheshimiwa Wabunge kupitia Bunge hili tuwasii watanzania na kuwataka wote wanaoishi mabondeni wahame kwasababu mvua hizi zinapokuja wanapata madhara makubwa na hatimaye sasa hata katika kuwaokoa inakuwa shida. Kwa hiyo ni vizuri sasa tukashirikiana".

Pamoja na hayo, Majaliwa ameendelea kwa kusema "serikali kwa upande wake inaanda fedha kuhakikisha kwamba ile miundombinu ya mabonde ina boreshwa ili maji yaweze kupita kwa ulaini. Lakini watu waliokaa katika mabonde na yale maeneo yote waliyokataziwa waanze kuondoka mapema ili wasiweze kupata madhara pindi mvua nyingi zinapojitokeza".

Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewapa pole wananchi wote walioweza kupata maafa ya aina yeyote yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya mkoa wa kigoma

 Mkoa wa Kigoma  uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Viwianishi: 4°53′S 29°40′E / 4.883°S 29.667°E Nchi Tanzania Wilaya 8 Mji mkuu Kigoma Serikali - Mkuu wa Mkoa Emmanuel Maganga Eneo - Mkoa 46,066 km² - Bara 37,037 km² - Maji 8,029 km² Idadi ya wakazi (2012) - 2,127,930 Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa K...

UK yawatahadharisha Watanzania Kuhusu Maandamano Ya Tarehe 26/04/2018

                London, Uingereza. Serikali ya Uingereza imewataka wananchi wake wanaoishi hapa nchini kuchukua tahadhari na maandamano ya kisiasa yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26. Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Aprili 24 imesema kwamba kuna raia zaidi ya 75,000 wanaoingia nchini hapa kila mwaka. Hivyo imewatahadharisha kujihusisha na maandamano hayo kwa madai kwamba wanaweza kupata madhara kutoka kwa jeshi la polisi. Katika taarifa hiyo ilitolewa tahadhari kwamba kwa sababu maandamano hayo yalishapigwa marufuku hivyo polisi ni lazima watatumia mabomu ya machozi au silaha za moto. “Hivyo muwe makini sana mnapokuwa kwenye mizunguko yenu muepuke mikusanyiko ya watu au watu wanaoandamana, muda wote muwe mnasikiliza vyombo vya habari, mjue nini kinachoendelea,’’ ilisema taarifa hiyo na kuongeza: “Ikiwa mnahitaji mawasiliano na namba ya dharura ya kupiga haraka ni 112 uliza huduma ya d...

Diamond Amtumia Salamu Ali Kiba Baada ya Kusikia Amefunga Ndoa

From Daimond "Ni Mwendo wa Picha za Suti tu sasa hivi, Maana nisije nikafungua hata kashati nikajikuta Centro...Pole yenu Wa zee wa Gym, Kama Muscat Round hii🤣🤣🤣.... Wadau Nimeambiwa King Kiba kaoa leo...Mfikishieni Salam zangu, za Ndoa njema, na Maisha yenye Furaha, Amani na Baraka tele...🔥🔥🔥 # SanaaImezaliwaUpya "