Skip to main content

Wema ampiga dongo Mange Kimambi kuhusu maandamano yake




Wema Sepetu amempiga dongo Mange Kimambi kufuatia maandamano aliyokuwa akiyahamasisha kupitia mitandao ya kijamii akiwataka Watanzania waandamane kutokufanikiwa. 

Mange alikuwa akiwashawishi Watanzania kuandamana leo katika maadhimisho wa miaka 54 ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni ishara ya kupinga baadhi ya mambo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano, lakini hata hivyo, maandamano hayo hayajafanyika katika kiwango kilichokuwa kikidhaniwa. 

Watu wengi leo walikaa majumbani mwao wakihofia kutoka nje kutokana na polisi kutishia kuwashughulikia wale wote watakaoandamana, hali iliyopelekea baadhi ya watu kukatisha shughuli zao. 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Wema amesema kuwa alisitisha safari yake ya kwenda Arusha kutokana na hofu kuwa kungekuwa na maandaamano, kumbe hakuna kitu chochote. 

“Watu Tukajua Kuna Maandamano mpaka Safari tukazihairisha… Kumbe hamna kitu… Ila utani tuweke pembeni wengi wetu tulishtushwa… But one thing y’all have to understand is Wa Moja Wa Moja tu… Aliepewa kapewa… And Kamwe huwezi shindana na POWER.” 

Aliendelea kusema, “ARUSHA… Tunaomba Radhi… We had to Cancel our Trip sababu ya Haya Mambo ya Uongo na Kweli… But Tunakuja Soon tutawajulisha wapendwa wetu.” 

Licha ya kuwa Wema hakumtaja Mange katika ‘post’ yake, lakini ni dhahiri kuwa dongo hili limeelekezwa kwa Mange kwani ndiye alikuwa mhamasishaji mkuu wa maandamano haya ambayo Wema amesema ni ya uongo.


Comments

Popular posts from this blog

Niyonzima Apata Ajali Ya Gari

Haruna Niyonzima KIUNGO wa Simba, Haruna Niyonzima amenusurika katika ajali aliyoipata eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam. Niyonzima amepata ajali hiyo juzi baada ya gari lake kupiga bonde na kupoteza mwelekeo wakati akirejea nyumbani kwake. Taarifa zinaeleza Niyonzima raia wa Rwanda alikuwa mwenyewe kwenye gari na akiwa njiani wakati anarejea nyumbani, akakutana na majanga hayo. Jana Championi  juhudi za kumpata Niyonzima aliyetua nchini kuichezea Yanga akitokea APR ya Rwanda na baada ya kumpata alithibitisha kupata ajali na kusema anamshukuru Mungu kwa kuwa haikuwa ajali kubwa. “Gari lilipoteza mwelekeo wakati nikiwa njiani narejea nyumbani na kuingia kwenye msingi. Bahati nzuri sikuwa katika mwendo mkubwa na kuna mtu alikatiza ghafla, nilipojaribu kumkwepa nikapoteza mwelekeo wakati najitahidi kurudi barabarani, nikapiga bonde gari likanishinda nikaingia msingini. “Haukuwa msingi mrefu, baadaye walikuja watu tukalitoa nikaondoka. Nashukuru sikuumia wala yule mtu sikumgonga

Rais Magufuli aitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ameipandisha hadhi Manispaa ya Mji wa Dodoma na kuwa Jiji, huku akimtaja Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma wa sasa kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo jipya. Dkt. Magufuli amesema hayo leo Alhamisi, Aprili 26, 2018 wakati akihutubia wananchi waliojitokeza katika Viwanja vya Jamhuri, Dodoma wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania. “Lengo la Serikali yetu kuhamia Dodoma lipo pale pale, hatuwezi kurudi nyuma. Sasa hivi zaidi ya watumishi 3,800 wameshahamia, mimi nitahamia Dodoma mwaka huu. Dodoma ndio Makao Makuu. Kwa mamlaka mliyonipa, natangaza rasmi kuanzia leo Aprili 26, 2018, Manispaa ya Dodoma itakuwa Jiji la Dodoma, mkurugenzi wake ataanza kuitwa Mkurugenzi wa Jiji”, amesema Dkt. Magufuli. Aidha, Rais Magufuli amesema maandalizi yote ya kisheria yaanze kutumika katika jiji hilo jipya nalitakuwa Jiji la kipekee kwa sababu lipo katikati ya Tanzania”.

Mama Kanumba Amjibu Wema Baada ya Kukataa Kuigiza Nae.

BAADA ya hivi karibuni staa wa filamu, Wema Sepetu kueleza maneno aliyoelezwa na aliyekuwa msanii wa filamu, marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake kwamba hataki kabisa mama yake mzazi, Flora Mtegoa aigize, mzazi huyo ameibuka na kufungukia ishu hiyo. Akipiga stori na Za Motomoto News, mama Kanumba alisema mwanaye huyo alisema hayo kwa sababu alikuwa akimtunza na kumlipa mshahara kama mfanyakazi lakini kwa sasa hayupo hivyo ndiyo maana ameingia kwenye sanaa ya uigizaji kwa kuwa bila hivyo angegeuka ombaomba jambo ambalo halipendezi. “Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha,” alisema mama Kanumba