Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2018

Stendi ya mabasi ya mikoani Ubungo kuhamishwa kupisha kituo cha mabasi ya Mwendo Kasi

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ipo kwenye majadiliano ya kuhamisha kituo cha Mabasi Yaendayo Haraka (UDART), kilichopo Jangwani na kukipeleka kwenye kituo cha Mabasi yaendayo Mikoani Ubungo (UBT). Hatua hiyo inatokana na eneo hilo la Jangwani kukumbwa na mafuriko ya mara kwa mara hali inayosababisha kuharibika kwa magari hayo. Akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha madiwani jana, Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, alisema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru magari hayo yasiendelee kuharibika. Alisema Menejimenti ya Kampuni ya UDART na viongozi wa jiji wapo kwenye majadiliano kuhusu suala hilo ili waweze kufikia mwafaka. “Kwa sasa tupo kwenye majadiliano kwa ajili ya kuhamisha kituo cha mabasi yaendayo kasi(UDART) cha Jangwani tuweze kukipeleka Ubungo kwa sababu eneo la Jangwani limekuwa likikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara mvua inaponyesha,” alisema Mwita. Alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Halmashauri ya Jiji hilo ipo kwenye mchakato wa kupanua Mt

Rais Trump kukutana na rais Moon Mei 22

Rais Donald Trump anatarajia kukutana na rais wa Korea Kusini Moon Jae In ifikapo 22 Mei.  Viongozi hao wawili watakutana katika ikulu ya White House nchini Marekani.  Msemaji wa White House Sarah Sanders ametoa maelezo kuhusu mkutano huo na kusema kuwa Korea Kusini ina uhusiano mzuri na Marekani.  Trump ambae natarajia kukutana na Moon kwa mara ya tatu sasa,anaamini mkutano huo utasaidia katika kudumisha mahusiano kati ya mataifa hayo amwili.  Trump vilevile anatarajia kukutana na Kim Jong Un hivi karibuni.

Mabasi ya Mwendokasi yasitisha huduma zake kwa muda

Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka (UDART) imeamua kusitisha usafirishaji wa abiria kwa baadhi ya njia kuanzia saa 6:00 mchana kutokana na kufungwa kwa barabara ya Morogoro eneo la Jangwani kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.  Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa na kusema wamechukua maamuzi hayo kutokana na maji mengi ya mvua kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam hali ambayo inahatarisha usalama wa abiria pamoja na vyombo vya usafirishaji.  "Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi - Kimara, Kimara - Morroco, Kimara - Magomeni Mapipa, Kivukoni - Muhimbili, Gerezani - Kvukoni, na Gerezani - Muhimbili. Huduma kamili zitarejea mara baada ya barabara kufunguliwa", amesema Bugaywa. Kwa upande mwingine, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART, Deus Bugaywa amewaomba radhi wananchi wanaotumia usafiri huo kwa usumbufu ambao utajitokeza kwa namna moja ama ny

Polisi abakwa alipokwenda kumkamata mbakaji

Askari Polisi mmoja wa kike huko  Yorkshire Kusini, nchini England  ameripoti kubakwa na mwanaume ambaye alikwenda kumkamata akiwa na askari mwingine kwa makosa ya jaribio la kubaka. Mwanaume huyo alikuwa akihisiwa kufanya vitendo hivyo vya  kujaribu kubaka watoto wa kike  na ndipo askari huyo alipokwenda na mwenzie kumkamata ili afikishwe polisi. Inaelezwa kuwa mwanamume huyo tayari amekwisha kamatwa na amefungulia mashtaka ya  kujaribu kubaka, shambulio, unyanyasaji wa kijinsia na uharibifu wa makosa ya jinai .

Rais Magufuli aomba msaada Serikali ya Denmark

Rais John Magufuli ameiomba Serikali ya Denmark kusaidia ujenzi wa kipande cha barabara ya kilomita 11 katika Mkoa wa Iringa ili kuwezesha malori kutopita katikati ya mji huo ikiwa ni pamoja na kupunguza ajali zinazotokea.  Rais Magufuli ombi hilo wakati akizindua barabara ya Iyovi – Iringa – Mafinga yenye urefu wa kilomita 218 iliyojengwa kwa mkopo nafuu kutoka serikali ya Denmark na kugharimu Sh283 bilioni.  Akitoa maelezo wakati akiomba msaada huo Dk. Magufuli amesema mpango huo ulikuwepo tangu alipokuwa wizara ya ujenzi na kufafanua kwamba malori yanayopita katikati ya mji wa Iringa yamekuwa yakisababisha ajali ndani ya mji wa huo.  “Nakuomba Balozi, hili mlichukue kama la urgent, mkitusaidia kama mkopo sisi tuko tayari, mkitupa kama msaada tutashukuru zaidi. Kwa hiyo tunaomba utufikishie hili, ikiwezekana barabara hiyo tutaiita Pamela Road,” amesema  Mbali na hayo Rais ameweka wazi kwamba "Ujenzi wa barabara hii umegharimu bilioni 283.71 nimekopa kutoka Denmark, mb

Mwita Waitara: Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure

Mbunge wa Ukonga (CHADEMA) Mh. Mwita Waitara amehoji uamuzi wa serikali kutangaza kutoa elimu bure licha ya changamoto ambazo bado zinaikumba sekta hiyo nchini na kutaka wananchi waingie gharama za kuchangia elimu isipokua kwa familia maskini.  Waitara amesema hayo jana bungeni Mei 02, 2018 wakati wa kuchangia bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kuongeza kwamba Tanzania hakuna elimu ya bure bali serikali imepunguza gharama kwa kufuta ada tu.  “Na mimi nimekua nikipinga mara zote Tanzania hakuna elimu ya bure, kuna elimu iliyopunguzwa gharama zake, serikali ilichofanya imeondoa ada lakini mambo mengine yatabaki, natukubaliane mheshimiwa Mwenyekiti haiwezekani taifa hili kila kitu kikatolewa bure watoto watakua wazembe na walemavu” alisema Waitara  Waitara ameongeza kuwa kitendo cha serikali kutangaza elimu bure kinadumaza wananchi na kushindwa kutimiza majukumu yao kama wazazi katika jukumu la kusimamia watoto kielimu na itapelekea Tanzania kuwa ni taifa la wat

Ajisalimisha Polisi baada ya Mzigo alioiba kunasa mabegani

KIJANA Frank Japhet (23), mkazi wa Mbezi, Dar es Salaam, amelazimika kujisalimisha katika Kituo cha Polisi Mlandizi, Kibaha, Pwani, baada ya mzigo wa mahindi unaokadiriwa kuwa na uzito wa kilogramu 20, anaodaiwa kuuiba kung’ang’ania mabegani.  Wakati akihojiwa kituoni hapo, mtuhumuwa huyo amesema mzigo huo, uliofungwa kwenye kiroba aliuiba kwa mama mmoja eneo la Mtaa wa Nyambwiro, Mlandizi, Kibaha, mkoani Pwani majira ya saa 7.00 usiku wa kuamkia leo Mei 3, 2018, akaongeza kwamba aliondoka na mzigo huo hadi eneo la Stendi ya Mlandizi alipokuwa auache kwa mwenzake ili arudie mzigo mwingine, ambapo mzigo huo uling’ang’ania kichwani.  Ameendelea kusema kwamba alijitahidi kufanya kila aliloweza ili mzigo huo utoke kichwani ikiwa ni pamoja na kulala ili akinyanyuka ubaki chini lakini aliponyanyuka, alinyanyuka nao kichwani! Baada ya kuzunguka nao kwa muda mrefu, alidai alichoka hivyo akalazimika kujisalimisha polisi ili asije akauawa na raia wenye hasira watakapobaini kuwa ni mwizi

Mwanamke aliyevuliwa chupi kanisani azungumza

  Siku moja tu baada ya picha za mwanamke mmoja kusambaa mitandaoni akitolewa chupi kanisani na jamaa aliyedaiwa kuwa pasta, mwanamke huyu amevunja kimya. Wengi walikishutumu kisa hicho huku uozo katika jamii ukibanika wazi. Baadhi wakidai kuwa mapasta hufanya lolote na hata kuwadhulumu na kukiuka haki za waumini kwa jina la kusuluhishia matatizo yao. ‘’ Hii ni movie wala si kanisa kama wengi wanavyodai, tafadhali komeni kueneza habari za uongo. Mimi ni muigizaji na ni jukumu langu kutoa lesoni kamili kwa ulimwengu.’’  Alibainisha Mwanamke muigizaji ambaye sasa ametambulika kama Piesie Asamoah Gifty kupitia kwa mtandao wake wa Facebook. Jaridala TUKO.co.ke limeweza kuthibitisha kuwa video hiyo ya kuigiza kina mada ‘Pastor Blinks’ na kitazinduliwa hivi karibuni. Mwandishi wa mchezo huo Trus Pleroma Nyowikech alivilaumu vikali vyombo vya habari kwa kueneza habari hiyo. Mwanamke huyo ameeleza kuwa huo ulikuwa mchezo wa kuigiza. ‘’ Kwa wale ambao hawakuamini nilipozichapisha baadhi

Mrithi wa Morgan Tsvangirai: Mkinichagua kuwa Rais nitawafukuza Wachina wote

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change (MDC) nchini Zimbabwe, Nelson Chamisa amesema kuwa atawafukuza wawekezaji wote kutoka China nchini humo endapo atachaguliwa kuwa Rais kwenye uchaguzi mkuu mwezi Julai mwaka huu.  Chamisa amesema kuwa Wachina wamekuwa wakitorosha rasilimali za nchi hiyo na uwekezaji wao umegubikwa na rushwa hivyo haoni sababu ya kuwaruhusu kufanya kazi nchini humo.  “Wawekezaji kutoka china ni moja ya watu wanaolifilisi taifa letu, wanachukua rasilimali zetu kwa kisingizio cha uwekezaji na wamesaini mikataba ya hovyo na serikali ya Zanu-PF sioni umuhimu wao ni bora tukaacha hizo rasilimali zikatumiwa baadae nawaahidi mkinichagua kuwa rais nitawafukuza wawekezaji wote Wachina na wengine ambao wataonekana na mikataba kama hiyo nitawatimua, tumechoka kunyonywa,“amesema Chamisa juzi Mei 01, 2018 mjini Harare kwenye maadhimisho ya siku yawafanyakazi duniani.  Zimbabwe inatajwa kuwa ni nchi ya nne barani Afrika kuwa na wawekezaji wengi ku