Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2018

Tundu Lissu Arejea d'salaam.

tundu lissu. Lissu ambaye amekuwa hospitalini tangu Septemba 7, mwaka jana aliposhambuliwa nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma, aliliambia shirika la utangazaji la BBC juzi, kuwa kwa sasa hana tena kidonda cha risasi na yupo tayari kurudi nyumbani. "Sina tena kidonda cha risasi, nilipigwa mara 16," alidai Lissu (50) na kufafanua "sina tena kiungo kilichovunjwa". "Nilikuwa nimevunjwa mguu mmoja mara tatu, mikono yote ilikuwa imevunjwa, nilikuwa na risasi nyingi mwilini, na vidonda vingi." Lissu ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, alisema viungo vyote vilivyokuwa vimevunjika vimeshaunga. Alisema tangu aanze kupata matibabu amefanyiwa operesheni 17, nne zikiwa sehemu ya tumbo, lakini sasa hali yake ni nzuri. Lissu alisema analazimika kurundi nchini kwa kuwa yeye ni Mbunge, Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Waziri kivuli wa Sheria na Katiba. Alisema kwa majukumu hayo hawezi kwenda mafichoni. "Siwezi kwenda mafichoni,

Lema Anena Maneno Mazito kwa Jeshi la Polisi

Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameandika katika ukurasa wake wa Twitter “ Kazi ya Polisi ni kazi zenye heshima ni kazi ya kujitolea kwa ajili ya wengine,” “Sura hii imepotea na kuna chuki kubwa ambayo ni hatari kwa ustawi wa nchi. Matukio dhidi ya raia yanaleta wasi wasi katika nchi. Kiongozi anayejali nchi hapaswi kuwa kipofu na asiweze kuona mambo haya” -ameandika Lema

Serikali: Haiwezekani Majuto Kuomba Sh 500,000

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amesema inaudhi kuona msanii wa filamu, Amri Athuman maarufu King Majuto anaomba msaada wa Sh 500,000 kwa ajili ya matibabu wakati kuna makampuni yalifaidika naye kwa kuingia mikataba aliyodai ya dhuluma. Kutokana na hali hiyo, amesema serikali imechoka kusikia vilio vya wasanii wa filamu kudhulumiwa haki zao na sasa imeunda kamati maalumu ya wanasheria kukagua mikataba yote ya mashirika na makampuni waliyoingia wasanii akiwamo  King Majuto na marehemu Seteven Kanumba ‘Kanumba’. Pia imeagiza wasanii wote ambao wanaona wameingia mikataba ya kipumbavu na makampuni au mashirika hayo wawasilishe taarifa zao kwa serikali. Dk. Mwakyembe amesema hayo Juzi Aprili 27, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja za wabunge katika kuhitimisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo. “Kwa kweli dhuluma kwa wasanii ilikuwapo kubwa sana kwa kutumia ‘middle men’ (watu wa kati), watu wenye fedha wamechezea sana Watanzania wetu. Hili lim

Tukio la Kuuawa Watoto 140 kwa Wakati Mmoja Kama Sadaka Lagundulika

Hivi karibuni wataalamu wamegundua kinachofikiriwa kuwa tukio kubwa zaidi la mauaji dhidi ya watoto kwenye historia ya dunia. Imegundulika kwamba zaidi ya watoto 140 waliuawa kama sadaka kwa wakati mmoja katika moja ya miji ya Pwani ya Kaskazini ya nchini Peru, takribani miaka 550 iliyopita. Inaelezwa pia sadaka ya watoto hao ilitolewa pamoja na aina ya miti ambayo ilikuwa michanga iliyojulikana kama Ilama siku hiyo hiyo waliouawa watoto. Mdogo wa Mbunge John Heche asababishiwa kifo kwa kuchomwa kisu Watoto hao 140 wanaelezwa kuwa walikuwa na umri wa kuanzia miaka mitano hadi 14 japokuwa wengi wao walikuwa kati ya miaka 8 hadi 12

John Heche Azungumza Mazito Baada ya Mdogo Wake Kuuwawa Kikatili na Polisi

Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche amefunguka kuwa mpaka sasa haelewi ni kwa vipi mtu anaweza kuuwawa na polisi kwa kuchomwa kisu tena akiwa amefungwa pingu huku akikumbushia tukio la mdogo wake mwingine kujeruhiwa vibaya na polisi ambapo alisababishiwa ulemavu mwaka jana.  Mbunge Heche amesema kwamba mtu kuchomwa kisu mgongoni ni kudhamiria kuua kwasababu mtu huyo hakuwa anapambana.  "Nilijua mikononi mwa polisi ni sehemu salama, wiki mbili zilizopita kijana Allen alikufa katika mazingira tata kule Mbeya, Mwanza mama aliyekamatwa na kunyimwa dhamana mtoto wake mchanga alikufa. Leo ni kwangu mdogo wangu ameuwawa kikatili sana mikononi mwa polisi. Maisha yangu yote nimeyatoa kupigania haki ili watu wasionewe, mtuhumiwa asifanywe mkosaji na kuhukumiwa kabla ya vyombo vya sheria kumhukumu,"  Heche.  Ameongeza " Mwaka jana mdogo wangu mwingine aliumizwa vibaya sana na polisi. IGP Mangu na RPC waliokuwa Tarime walilipa uzito suala hilo lakini walipoondolewa, sual

Waziri Shonza Afunguka suala la Kufungiwa kwa 'Mwanaume Mashine'

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema wimbo wa Mwanaume Mashine haujafungiwa.  Ametoa kauli hiyo leo jioni Aprili 27, 2018 baada ya leo mchana Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuhoji sababu za kufungiwa kwa wimbo huo.  Shonza ametoa kauli hiyo wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19 baada ya Zungu kutaka kupewa jibu kuhusu ‘Mwanaume Mashine’ kutokana na maelezo ya Shonza na Waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe wakati wanajibu hoja za wabunge kuhusu bajeti hiyo kutoeleza sababu za kufungiwa kwa wimbo huo.  Mchana Zungu alihoji kufungiwa kwa wimbo huo wakati unamtaja mchezaji mahiri wa Simba.  Bunge limepitisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo mwaka 2018/19

Ridhiwani Kikwete Afunguka Kuhusu Kifo cha Mdogo wa Mbunge John Heche Kilichosababishwa na Polisi

Ridhiwani Kikwete Afunguka Kuhusu Kifo cha Mdogo wa Mbunge John Heche Kilichosababishwa na Polisi  @ridhiwani_kikwete - Kitendo kilichotokea sio tu kimesikitisha ukoo wa Bwana Heche lakini kwangu Binafsi. Jeshi letu limetengenezwa kulinda Watu na Mali zao sio kuumiza wasio na hatia. Ni imani yangu Serikali itasimamia haki kwa familia ya Heche. Poleni sana kwa Msiba.Mungu awape subira @HecheJohn

Mama Kanumba Amjibu Wema Baada ya Kukataa Kuigiza Nae.

BAADA ya hivi karibuni staa wa filamu, Wema Sepetu kueleza maneno aliyoelezwa na aliyekuwa msanii wa filamu, marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake kwamba hataki kabisa mama yake mzazi, Flora Mtegoa aigize, mzazi huyo ameibuka na kufungukia ishu hiyo. Akipiga stori na Za Motomoto News, mama Kanumba alisema mwanaye huyo alisema hayo kwa sababu alikuwa akimtunza na kumlipa mshahara kama mfanyakazi lakini kwa sasa hayupo hivyo ndiyo maana ameingia kwenye sanaa ya uigizaji kwa kuwa bila hivyo angegeuka ombaomba jambo ambalo halipendezi. “Kanumba alisema hayo kwa kuwa alikuwa ananitunza yaani ananinunulia vyakula na kunilipa mshahara kila mwezi kama mfanyakazi lakini sasa hayupo, je Wema alitaka nishike bakuli nikaombe barabarani au? Maana kulima siwezi hivyo naona tu bora niigize ili niweze kujikimu kimaisha,” alisema mama Kanumba

Kanuni Mpya Kudhibiti Matusi na Picha za Uchi Mitandaoni

Serikali imesema kanuni mpya za maudhui kwenye mitandao, runinga na redio zimetungwa kwa lengo la kudhibiti usambazaji wa kauli chafu, matusi, picha za utupu na zenye maudhui yasiyofaa kwa watoto. Kanuni hizo zimetungwa ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kiektroniki na Posta ya Mwaka 2010. Pia imesema itaendelea kuhamasisha utengenezaji na uzalishaji wa maudhui ya ndani yanayozingatia maadili, mila na desturi za Mtanzania huku ikikiri kuwapo kwa mmomonyoko wa maadili kunakoongezeka siku hadi siku, hivyo imejipanga kukabiliana na changamoto hiyo. Akiwasilisha bungeni mjini hapa jana hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Waziri wa wizara hiyo, Dk. Harrison Mwakyembe, alisema kanuni hizo zinamtaka kila mtumiaji wa mitandao awe na namba ya siri ili 'wajanja' wasitumie kirahisi chombo chake cha mawasiliano kutenda matendo yanayokwenda kinyume cha sheria. Alisema kanuni hizo pia zinaweka muda maalumu kwa picha mgando

AJALI YAUWA WATATU KAGERA

Watu watatu wamefariki papo hapo baada ya kugongwa na gari aina ya basi Frester lenye namba za usajili T.720 DEV eneo la Katongo kata ya Rulanda wilayani Muleba mkoani Kagera asubuhi hii ya leo Miili haijatambulika watu hao ni vijana walikuwa wakienda madrasa ambapo basi hilo lilikuwa likitokea Bukoba kwenda Mwanza Kwa mujibu wa abiria waliokuwa kwenye basi hilo wamesema dreva alitaka kumkwepa mwendesha bodaboda na kuwaparamia vijana hao akiwemo huyo bodaboda na kusababisha gari kupinduka Aidha abiria waliojeruhiwa wanaokolewa na wenzao kwani viungo vya miili vimenasa kwenye vyuma huku zikifanyika jitihada za kuwapeleka kituo cha afya kaigara na hospitali ya Rubya wilayani Muleba. Hali ya hewa katika eneo hilo kulikuwa pia na ukungu ulioambatana na mvua  inadaiwa basi lilikuwa mwendo kasi likitangulia mengine yaliyokuwa yakienda mikoani.

Irene Uwoya, Dogo Janja waikimbia nyumba

STAA  mkali wa filamu Bongo, Irene Uwoya na baby wake Abdul Chende ‘Dogo Janja’ wamefungukia dhamira yao ya kuihama nyumba waliyokuwa wakiishi na marehemu Agness Gerald ‘Masogange’ iliyopo Makongo Juu jijini Dar wakidai kuwa, hawatakuwa na amani. Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa niaba ya mkewe, Dogo Janja alisema kuwa hawawezi kuendelea kuishi hapo tena kwa sababu kwao itakuwa ni majonzi kila siku na hiyo ni kutokana na ukaribu waliokuwa nao kwa Masogange. “Kwa kweli mimi na mke wangu hatuwezi tena kuendelea kuishi Makongo Juu kwenye ile nyumba maana kwetu itakuwa ni simanzi tuu, Masogange alikuwa ni mtu wetu wa karibu sana na tulikuwa tukifanya vitu vingi pamoja, pia mke wangu atakuwa na huzuni sana akiendelea kuishi pale,” alisema Dogo Janja.

MAGAZETI YA LEO 28/4/2018

TANZIA : ABBAS KANDORO AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba Mkuu wa mkoa mstaafu Mzee Abbas kandoro amefariki dunia usiku huu wa Ijumaa Aprili 27,2018 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es salaam alikolazwa kwa matibabu. M/mungu Ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. AMIN Taarifa zaidi tutawaletea hivi punde

Azamu Yafuata Nyayo za Simba, Yanga

Klabu ya soka ya Azam FC imetua mkoani Morogoro kwaajili ya kuweka kambi kuelekea mchezo wake dhidi ya Mtibwa Sugar, utakaopigwa kesho huku pia klabu za SImba na Yanga zikiwa zimeweka kambi mkoani humo. Azam FC imeondoka jijini Dar es salaam ikiwa tayari imeshafanya maandalizi yote ya mchezo huo na kitakachofanyika katika kambi ya muda mfupi Morogoro ni mazoezi mepesi tu kabla ya mechi. Jumanne hii Azam FC ilicheza mchezo wa kirafiki na Kombaini ya Jeshi na kushinda mabao 2-0 yaliyofungwa na mshambuliaji Shaaban Idd na winga Enock Atta. Mchezo huo ulikuwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya kesho. Timu hizo zilipokutana kwenye raundi ya kwanza zilitoka sare ya bao 1-1, Azam FC ikitangulia kufunga kupitia kwa winga Enock Atta kabla ya Kelvin Sabato kusawazisha dakika za mwisho kwa mpira wa moja kwa moja wa adhabu ndogo. Hadi sasa kwenye msimamo wa ligi, Azam FC inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 46 huku wapinzani wao Mtibwa Sugar ikiwa nafasi ya sita kwa pointi 33. S

Hatimae Gigy Money Ajifungua Mtoto wa Kike

Mwanadada wa bongo fleva na video Queen Gift Stamford Gigy money amejifungua mtoto wa kike usiku wa kuamkia leo ambaye amezaa na mpenzi wake wa muda mrefu Moj ambaye ni mtangazaji wa choice fm. Moj na Gigy Money kabla ya kupata mtoto huyo walikuwa wakitaniana kwa kuitana mama Candy na Baba Candy amefunguka na kudai kuwa mtoto wao hawatampa jina hilo bali wataangalia jina lingine la kumwita.

Tundaman aweka sababu iliyomfanya akae Kimya

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tunda Man, amesema sababu iliyomfanya awe kimya baada ya kuoa ni kutafuta heshima ya ndoa, ambayo alihisi asingeipata kwa mapema angedhalilika. Akizungumza na eNewz ya East Africa Television, Tunda Man amesema kwamba kitendo cha kutokuwa na mtoto baada ya kuoa kilikuwa kinamnyima raha, hivyo aliamua aache vingine vyote ili kutafuta heshima ya ndoa, lakini sasa anarudi kwenye game rasmi kwani ameshapata alichokuwa akikitafuta. “Kitu kikubwa ni kwamba sasa niko huru, mwanzo ilikuwa heshima ya ndoa lazima mtoto, kitu kama hiko kilikuwa kinanitia stress kinoma yani, kwa hiyo nimeoa kama miaka miwili iliyopita, na nilikuwa nimekaa kimya ka muda mrefu kutafuta heshima ya ndoa, mnielewe wananchi, nafikiri heshima imekuja tayari, nina mtoto anaitwa Itsal, kwa hiyo kitu kikubwa sasa hvi nadeal na ngoma zangu”, amesema Tunda Man. Msanii huyo amesema wiki ijayo anatarajia kuachia kazi mpya tatu kwa pamoja, ikiwemo ambayo ametunga baada ya kushuhudia mach

Mwenyekiti Bavicha mbeya ashikiliwa na Polisi

Mbeya.  Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) Mkoa wa Mbeya, George Titho amekamatwa na polisi usiku wa manane nyumbani kwake kijijini Kyimo wilayani Rungwe. Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mussa Taibu alipoulizwa na MCL Digital kuhusu kukamatwa kiongozi huyo, amesema hana taarifa. "Sina taarifa hizo, labda nifuatilie lakini jua tu kwamba hali Mbeya ni shwari," amesema Kamanda Taibu. Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Boid Mwabulanga amesema Titho alikamatwa usiku wa kuamkia Aprili 26, 2018. Mwabulanga amesema hawajaambiwa sababu za kukamatwa kwa Titho na jitihada za kumwekea dhamana zimegonga mwamba. "Walikwenda nyumbani kwake saa nane usiku na kuvunja mlango, wakachukua simu zake kisha wakamchukua kwenda naye kituo cha polisi Tukuyu. Tumekwenda asubuhi kumwekea dhamana lakini walikataa,” amesema.

Wema ampiga dongo Mange Kimambi kuhusu maandamano yake

Wema Sepetu amempiga dongo Mange Kimambi kufuatia maandamano aliyokuwa akiyahamasisha kupitia mitandao ya kijamii akiwataka Watanzania waandamane kutokufanikiwa.  Mange alikuwa akiwashawishi Watanzania kuandamana leo katika maadhimisho wa miaka 54 ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni ishara ya kupinga baadhi ya mambo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano, lakini hata hivyo, maandamano hayo hayajafanyika katika kiwango kilichokuwa kikidhaniwa.  Watu wengi leo walikaa majumbani mwao wakihofia kutoka nje kutokana na polisi kutishia kuwashughulikia wale wote watakaoandamana, hali iliyopelekea baadhi ya watu kukatisha shughuli zao.  Kupitia ukurasa wake wa Instagram Wema amesema kuwa alisitisha safari yake ya kwenda Arusha kutokana na hofu kuwa kungekuwa na maandaamano, kumbe hakuna kitu chochote.  “Watu Tukajua Kuna Maandamano mpaka Safari tukazihairisha… Kumbe hamna kitu… Ila utani tuweke pembeni wengi wetu tulishtushwa… But one thing y’all have to understand is Wa Moja Wa Moja t

Serikali Yatarajia kununua ndege kubwa ya masafa marefu

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa Serikali inatarajia kununua ndege nyingine kubwa ya saba ya masafa marefu na kueleza kuwa haitakodi kwa sababu kukodi ni gharama kubwa ikilinganishwa na kununua. Prof. Mbarawa amesema Serikali haikurupuki kununua ndege hizo kwa kuwa inao mpango kazi unaobadilishwa kila mara kulingana na wakati. Ameendelea kwa kueleza kuwa nia ya serikali ni nzuri kwani huwezi kuwa na viwanja vya ndege kama huna shirika lako la ndege, hivyo serikali imenunua ndege sita ambazo tatu zimetua na zinafanya kazi. “Mwaka huu tunategemea ndege tatu zitawasilisha ambazo ni Boeng 787 ya masafa marefu yenye uwezo wa kuchukua abiria 262, nyingine mbili zenye uwezo wa kuchukua abiria 132 kila moja ni Bombardier CHCS 300 ambazo zitawasilia na kuanza kufanya kazi,” amesema. “Kikawaida huwezi kuwa na ndege moja ya masafa marefu ikafanya kazi vizuri hivyo kwenye bajeti hii tumeshapanga kununua ndege nyingine boeng 787 ili tuwe na n

Rais Magufuli atoa msamaha kwa wafungwa 3,319

Katika kuadhimisha miaka 54 ya Muungano, Rais wa Jamuhuri ya Muungno wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,319. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mamba ya Ndani, imesema kati ya wafungwa hao 585 wataachiwa huru leo na 2,734 wamepunguziwa adhabu zao na wataendelea kubaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo chao kilichobakia.

Rais Magufuli aitangaza Manispaa ya Dodoma kuwa Jiji

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ameipandisha hadhi Manispaa ya Mji wa Dodoma na kuwa Jiji, huku akimtaja Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma wa sasa kuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo jipya. Dkt. Magufuli amesema hayo leo Alhamisi, Aprili 26, 2018 wakati akihutubia wananchi waliojitokeza katika Viwanja vya Jamhuri, Dodoma wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania. “Lengo la Serikali yetu kuhamia Dodoma lipo pale pale, hatuwezi kurudi nyuma. Sasa hivi zaidi ya watumishi 3,800 wameshahamia, mimi nitahamia Dodoma mwaka huu. Dodoma ndio Makao Makuu. Kwa mamlaka mliyonipa, natangaza rasmi kuanzia leo Aprili 26, 2018, Manispaa ya Dodoma itakuwa Jiji la Dodoma, mkurugenzi wake ataanza kuitwa Mkurugenzi wa Jiji”, amesema Dkt. Magufuli. Aidha, Rais Magufuli amesema maandalizi yote ya kisheria yaanze kutumika katika jiji hilo jipya nalitakuwa Jiji la kipekee kwa sababu lipo katikati ya Tanzania”.

Kiongozi wa Kidini Ahukumiwa Maisha Kisa Mamilioni ya Waumini

Mwanaume mmoja ambaye anadaiwa kuwa kiongozi wa kidini nchini India na kudai kuwa na mamilioni ya waumini dunia nzima, amehukumiwa kifungo cha maisha jela. Mwanaume huyo Asaram Bapu ambaye anatajwa kuwa na umri wa miaka 77 amehukumiwa kifungo cha maisha kwa kosa la kumbaka mtoto wa kike wa umri wa miaka 16. Bapu anaripotiwa kufanya kitendo hicho mwaka 2013 na anatuhumiwa mara nyingi kufanya vitendo hivyo vya ubakaji.

Wanawake Wapewa Adhabu ya Kuchimba Kaburi na Kijiji

Ni kawaida na ni utamaduni wa sehemu nyingi duniani wanaume kuchimba kaburi na kuwaachia wanawake shughuli nyingine za jikoni wakati wa msiba. Lakini sivyo ilivyokuwa kwa wanawake wa Mtaa wa Bwihegule wilayani Geita. Wanawake hao wa Kata ya Mtakuja walilazimika kuchimba kaburi, ikiwa ni adhabu iliyotokana na tuhuma kuwa wanahusika na vifo vya ghafla vya wanaume mtaani hapo. Tukio hilo lililoibua hisia na maoni mchanganyiko kutoka kwa walioshuhudia lilitokea Aprili 24 baada ya mkazi wa mtaa huo, Nkangiko Vigume (57), kufariki dunia ghafla Aprili 23. Wanaume saba wafariki Habari kutoka mtaani hapo zinasema amri ya kutaka wanawake kuchimba kaburi na kulala matanga ilitolewa na mtemi, ambaye ni kiongozi wa mila wa jamii ya Wasukuma mtaani hapo, Kahema Nsabilando. Alitoa amri hiyo baada ya uamuzi kufikiwa kwenye kikao cha dharura kilichojadili matukio ya vifo vya ghafla vya wanaume mtaani hapo. Wakazi waliitisha kikao hicho kujadili vifo vya ghafla vya wanaume baada ya Vigume k

Binti wa Miaka 20 Amuua Mdogo Wake na Kumficha Uvunguni

Binti wa miaka 20 ambaye jina lake halikutajwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi Temeke jijini Dar es salaam kwa tuhuma za kumuua mtoto wa miaka miwili, ambaye ametajwa ni mdogo wake na kisha kumficha uvunguni mwa kitanda huko nyumbani kwao Kigamboni jijini Dar es salaam. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Temeke Emmanuel Lukula amesema tukio hilo limetokea Jumatatu ya April 23, ambapo binti huyo alimchoma na kitu chenye ncha kali sehemu ya kitovu mtoto huyo na kumlaza kifudi fudi, kisha kutokomea kwa mpenzi wake. “Ni kweli tukio hilo limetokea,aliyefanya hilo tukio ni binti wa miaka 20 ambaye ni ndugu wa mama wa marehemu, alimchoma huyo mtoto na kumlaza kifudifudi uvunguni kisha akaondoka kwa mwanaume anayedaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi, na baada ya mama wa mtoto kurudi kazini hakumkuta nyumbani”, amesema Kamanda Lukula. Kamanda Lukula ameendelea kueleza kwamba baada ya hapo mama alitoa taarifa polisi, na baada ya uchunguzi walimkamata binti huyo na kuonyesh

Alichokisema Mange Kimambi Baada ya Idriss Kuandika Hivi Kuhusu Maandamano ya April 26 "Maandamano ya Amani Juu ya Jambo Fulani Yanahaki ya Kuungwa mkono"

Idriss Sultani ameonekana kuwa upande ambao umemfurahisha mwanaharakati mange Kimambi kuhusu kuweka msimamo wake juu ya maandamano yaliopangwa kufanyika siku ya kesho april 26 huku muandaaji mkubwa wa maandamano hayo akiwa mwanadada mange Kimambi.   Kupitia Ukrasa wake wa instagram Idriss aliandika "Maandamano yoyote yernye amani na ni kwaajili  ya kuweka awereness  juu ya jambo flani bila vita wala ugomvi wa aina yoyote  yana haki ya kupewa sapport  kama yamekugusa. Inaitwa the Democratic Republic on Tanzania. Let's  act like our name. Kuwa mzalendo kwa kuepuka maandamano ya shari tu Rismillah itangulie#mzalendo"  Baada ya Mange Kimambi kuona post ya Idriss naye aliandika hivi " Idriss uwezi kuelewa uzito wa post hii sababu watanzania wanahitaji  sapoti kama hii kutoka kwa nyinyi mastaa ni wewe pekee umejirisk  kwaajili yao. watanzania wanaweza  wasikulipe ila mungu atakulipa. Ulichokifanya leo  kina uzito wake. Idriss naomba usikae nyumbani siku ya leo......

Kampuni ya Maxcom Yaishtaki UDA-RT

  Kampuni ya Maxcom Africa PLC imeeleza kuwa, imefungua kesi ya madai katika Mahakama Kuu ya Tanzania dhidi ya Kampuni ya UDA-RT inayotoa huduma ya usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi, kutokana na kampuni hiyo kushindwa kulipa gharama za uendeshaji, uwekezaji na stahiki za wafanyakazi.

Watoto wa Miaka 14 na 15 Waoana kwa Idhini ya Mahakama ya Dini

Kutoka nchini Indonesia, watoto wawili, mvulana akiwa na miaka 15 na msichana miaka 14 jana April 24, 2018 wamefunga ndoa baada ya kupewa ruhusa kisheria kufanya hivyo.  Inaelezwa kuwa watoto hao walikwenda kutafuta ruhusa kwenye mahakama ya kidini ambapo inaelezwa kuwa serikali huwa haitoi ruhusa ya watoto kuoana mpaka mahakama ya kidini itoe ruhusa.  Walichoandika mastaa baada ya Meek Mill kuachiwa  Kesi ya watoto hiyo imekabiliwa na upinzani mkubwa ndani na nje ya nchi hiyo huku serikali ikipanga kufanya mabadiliko ya sheria.  Indonesia ni nchi yenye idadi kubwa ya Waislamu na wasichana wake wengi wadogo wameolewa.  Ushauri wa Halima Bulembo kwa Wapinzani “hawana hoja”  Sheria ya nchi hiyo kuhusu ndoa ni kwamba, msichana kuanzia miaka 16 na mvulana miaka 19 na kuendelea wanaweza kuoana lakini wanaweza kuoana hata chini ya umri huo kama mahakama ya kidini itaidhinisha.

Young Killer: Sasa hapo nibadilike nini

Rapa anayefanya poa kwenye gemu la Muziki wa Hip Hop Bongo, Erick Msodoki ‘Young Killer’, amekuwa akiambiwa mara kadhaa na mashabiki wake abadilishe aina ya ‘kuchana’, ameibuka na kukataa kutekeleza hilo kwani ameona hakuna sababu ya kufanya hivyo. Akizungumzia na Risasi Vibes, rapa huyo anayetamba na video ya Wimbo wa Shots, aliyom-shirikisha Khaligraph Jones kutoka Kenya, alisema kwamba hakuna maana kwani bado anaendelea na staili ileile ambayo inampatia hadi shoo zaidi ya tisa kwa mwezi. “Sasa hapo nibadilike nini. Mtu unayepata shoo nyingi inaonesha wazi kwamba unakubalika. Siwezi kubadilika na nitaendelea kukimbiza zaidi na zaidi,” alisema Young Killer.